• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    UCHANGANUZI WA KIMOFOFONOLOJIA WA MANENO-MKOPO YA KIMBEERE KUTOKA LUGHA YA KISWAHILI

    Thumbnail
    View/Open
    Wangari Kithaka.pdf (868.4Kb)
    Date
    2023-12
    Author
    KITHAKA, WANGARI
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Utafiti huu umechanganua kimofofonolojia maneno-mkopo ya lugha ya Kimbeere kutoka lugha ya Kiswahili ili kutambua nomino- mkopo na vitenzi- mkopo vya asili ya Kiswahili katika lugha ya Kimbeere. Malengo ya utafiti huu ni; kutambulisha nomino- mkopo na vitenzi-mkopo vilivyotoka lugha ya Kiswahili na kuingizwa katika lugha ya Kimbeere, kufafanua mifanyiko ya kimofofonolojia iliyohusika katika ukopaji wa nomino-mkopo na vitenzi- mkopo vya Kiswahili na kuingizwa katika Kimbeere na kubainisha kanuni za kiisimu zinazoongoza ukopaji wa nomino na vitenzi vya Kiswahili katika lugha ya Kimbeere.Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia (FZA) inayoangaziwa na Hooper (1976). Utafiti huu ni wa nyanjani na maeneo ya utafiti yaliyoteuliwa ni Ishiara, Kanyuambora, Kamumu, Ugweri na Siakago. Data ya kimsingi ya utafiti huu ilikuwa nomino-mkopo na vitenzi-mkopo vya lugha ya Kimbeere vinavyotokana na lugha ya Kiswahili. Nomino na vitenzi hivyo vilitokana na shughuli mbalimbali za maduka ya chakula, plastiki na mboga. Mbinu iliyotumika katika ukusanyaji wa data ni Uchunguzi Shiriki. Mbinu hii ilimbidi mtafiti aende nyanjani na kufanya kazi kama mhudumu madukani kwa muda wa wiki moja katika kila duka. Katika ukusanyaji data wake, mtafiti alinakili nomino-mkopo na vitenzi-mkopo kwenye daftari moja kwa moja kutoka kwa wazungumzaji waliofika madukani. Kurekodi sauti za wazungumzaji pia kulihusika katika ukusanyaji wa data. Hii ilimwezesha mtafiti kunasa matamshi mahsusi ya nomino-mkopo na vitenzi-mkopo zilizokusanywa. Baada ya kukusanywa, data ilichanganuliwa kwa kuzingatia hatua mahsusi. Kwanza mtafiti aliteua idadi ya watu kumi wenye umri wa kati ya miaka sitini na sabini ambao ni wazawa na wanaojua lugha ya Kimbeere vizuri ili kubaini maneno ya kukopwa na yasiyo ya kukopwa. Mtafiti kisha aliziweka nomino-mkopo na vitenzi- mkopo katika makundi. Baadaye nomino-mkopo na vitenzi-mkopo hivyo viliweza kunukuliwa kifonetiki. Mabadiliko ya sauti katika nomino-mkopo na vitenzi-mkopo hivyo kisha yalitambuliwa na sauti mahsusi zilizobadilika kuweza kuthibitishwa. Baadaye ruwaza za mabadiliko ya fonimu zilizotambuliwa na hatimaye kanuni zinazotawala michakato mahsusi ya kimofofonolojia ziliwekwa bayana.Utafiti huu una mchango mkubwa katika kuikuza lugha ya Kimbeere kwa sababu lugha hukua kadri inavyofanyiwa utafiti. Utafiti huu pia unaendeleza taaluma ya isimu linganishi kwani unahusu lugha ya Kiswahili na Kimbeere na mwingiliano wazo. Aidha, utafiti huu unakuza elimu ya isimu ya lugha za Kiafrika pamoja na kuendeleza elimu ya upataji lugha.
    URI
    http://elibrary.pu.ac.ke/handle/123456789/1198
    Collections
    • Department of Linguistics, Languages and Literature

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV
     

     

    Browse

    All of PUSpaceCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV