Show simple item record

dc.contributor.authorSwaleh, Rukiya Harith
dc.date.accessioned2020-09-28T11:29:50Z
dc.date.available2020-09-28T11:29:50Z
dc.date.issued2017-11-08
dc.identifier.other2017
dc.identifier.urihttp://elibrary.pu.ac.ke/handle/123456789/709
dc.descriptionTasnifu hii inahusu uchanganuzi wa kiufafanuzi wa kimofosintaksia wa njeo, hali na dhamira katika kitenzi cha Kitikuu. Njeo, hali na dhamira ni kategoria za kisarufi zinazopatikana katika kitenzi. Kitikuu ni lahaja mojawapo kati ya lahaja za Kiswahili. Kitenzi cha Kitikuu kina uwezo wa kubeba mofimu anuwai zenye uamilifu wa aina mbalimbali. Kati ya mofimu zinazopatikana katika kitenzi cha Kitikuu ni mofimu za njeo, hali na dhamira. Njeo ni kategoria ya kisarufi inayohusu uhusiano wa kiwakati wa kutendeka kwa tendo hasa kwa kurejelea wakati wa sasa. Hali nayo huangalia jinsi kitendo husika kinavyotendeka na wakati na kueleza kutimilika au kutotimilika kwa kitendo hicho. Nayo dhamira huonyesha nia au lengo la msemaji kama ni kuarifu, kuamuru, kusihi na kadhalika. Madhumuni ya utafiti huu ni kuelezea na kuainisha njeo, hali na dhamira katika lahaja ya Kitikuu na kuonyesha muingiliano wake katika lahaja hii. Nadharia ya Uminimalisti imetumika kuonyesha jinsi ukaguzi wa sifa unavyofanya kazi kwa vipashio hivyo vya njeo, hali na dhamira. Sentensi anuwai zenye kutumia mofimu hizo zimeonyeshwa na mifano ya uchanganuzi ya baadhi za sentensi, kwa kutumia nadharia ya Uminimalisti. Kulingana na Uminimalisti mofimu za njeo, hali na dhamira hupachikwa katika kitenzi kupitia mchakato wa kimkokotoo. Leksika za vitenzi na nomino hupewa mofimu zao katika leksikoni. Numerali huchagua sifa za kimofosintaksia za lugha fulani, baadaye muungano hutokea kwa kuunganisha chembechembe mbalimbali za lugha na kuunda maneno, virai na sentensi, hivyo kuunda miundo. Usogezi hutokea panapokuwa na haja, kwani usogezi huchochewa na haja za kimofosintaksia. Kitikuu kwa sababu ni lugha ambishi bainishi yenye ukwasi wa mofolojia, huruhusu usogezi ili kukagua sifa za uzalishaji kuhakikisha ukubaliano na mahali pa kisintaksia katika sentensi. Mofimu za njeo, hali na dhamira katika kitenzi cha Kitikuu hukaguliwa katika sehemu vi mbalimbali kuangazia ukubaliano wa kisarufi ili zisionekane katika umbo la kifonetiki (UF). Data juu ya njeo, hali na dhamira ilikusanywa kutoka maeneo ya Kizingitini, Tchundwa na Rasini, kwa watu wasiopungua umri baina ya miaka 45 hadi 70. Mtafiti pia alitumia umilisi wake alionao kuhusu lahaja hii ya Kitikuu, kama data msingi. Data ya ziada ni ya kutoka maktabani, ambapo upekuzi wa maktabani ulifanywa kuhusu lahaja ya Kitikuu, nadharia ya Uminimalisti na sarufi ya Kiswahili Sanifu. Kitikuu kina njeo mbili kuu: njeo iliyopita {li} na njeo ijayo {ta}. Kitikuu, kwa nadra hutumia njeo iliyopo {a} hasa katika vitenzi visaidizi. Kwa upande wa hali imegawanywa katika hali timilifu na hali isiyo timilifu. Hali timilifu hutumia mofimu {ndo} na {ie}. Hali isotimilifu hugawika katika hali mbalimbali kama hali ya mazoea {hu}, hali ya mfululizo {ka} na hali ya kuendelea {hu} na {ki}. Kuna dhamira mbalimbali zinazoonyeshwa kwa mofimu za kiishio {a} na {e} na dhamira za masharti zikionyeshwa kwa mofimu {ki} na {ngali}.en_US
dc.description.abstractTasnifu hii inahusu uchanganuzi wa kiufafanuzi wa kimofosintaksia wa njeo, hali na dhamira katika kitenzi cha Kitikuu. Njeo, hali na dhamira ni kategoria za kisarufi zinazopatikana katika kitenzi. Kitikuu ni lahaja mojawapo kati ya lahaja za Kiswahili. Kitenzi cha Kitikuu kina uwezo wa kubeba mofimu anuwai zenye uamilifu wa aina mbalimbali. Kati ya mofimu zinazopatikana katika kitenzi cha Kitikuu ni mofimu za njeo, hali na dhamira. Njeo ni kategoria ya kisarufi inayohusu uhusiano wa kiwakati wa kutendeka kwa tendo hasa kwa kurejelea wakati wa sasa. Hali nayo huangalia jinsi kitendo husika kinavyotendeka na wakati na kueleza kutimilika au kutotimilika kwa kitendo hicho. Nayo dhamira huonyesha nia au lengo la msemaji kama ni kuarifu, kuamuru, kusihi na kadhalika. Madhumuni ya utafiti huu ni kuelezea na kuainisha njeo, hali na dhamira katika lahaja ya Kitikuu na kuonyesha muingiliano wake katika lahaja hii. Nadharia ya Uminimalisti imetumika kuonyesha jinsi ukaguzi wa sifa unavyofanya kazi kwa vipashio hivyo vya njeo, hali na dhamira. Sentensi anuwai zenye kutumia mofimu hizo zimeonyeshwa na mifano ya uchanganuzi ya baadhi za sentensi, kwa kutumia nadharia ya Uminimalisti. Kulingana na Uminimalisti mofimu za njeo, hali na dhamira hupachikwa katika kitenzi kupitia mchakato wa kimkokotoo. Leksika za vitenzi na nomino hupewa mofimu zao katika leksikoni. Numerali huchagua sifa za kimofosintaksia za lugha fulani, baadaye muungano hutokea kwa kuunganisha chembechembe mbalimbali za lugha na kuunda maneno, virai na sentensi, hivyo kuunda miundo. Usogezi hutokea panapokuwa na haja, kwani usogezi huchochewa na haja za kimofosintaksia. Kitikuu kwa sababu ni lugha ambishi bainishi yenye ukwasi wa mofolojia, huruhusu usogezi ili kukagua sifa za uzalishaji kuhakikisha ukubaliano na mahali pa kisintaksia katika sentensi. Mofimu za njeo, hali na dhamira katika kitenzi cha Kitikuu hukaguliwa katika sehemu vi mbalimbali kuangazia ukubaliano wa kisarufi ili zisionekane katika umbo la kifonetiki (UF). Data juu ya njeo, hali na dhamira ilikusanywa kutoka maeneo ya Kizingitini, Tchundwa na Rasini, kwa watu wasiopungua umri baina ya miaka 45 hadi 70. Mtafiti pia alitumia umilisi wake alionao kuhusu lahaja hii ya Kitikuu, kama data msingi. Data ya ziada ni ya kutoka maktabani, ambapo upekuzi wa maktabani ulifanywa kuhusu lahaja ya Kitikuu, nadharia ya Uminimalisti na sarufi ya Kiswahili Sanifu. Kitikuu kina njeo mbili kuu: njeo iliyopita {li} na njeo ijayo {ta}. Kitikuu, kwa nadra hutumia njeo iliyopo {a} hasa katika vitenzi visaidizi. Kwa upande wa hali imegawanywa katika hali timilifu na hali isiyo timilifu. Hali timilifu hutumia mofimu {ndo} na {ie}. Hali isotimilifu hugawika katika hali mbalimbali kama hali ya mazoea {hu}, hali ya mfululizo {ka} na hali ya kuendelea {hu} na {ki}. Kuna dhamira mbalimbali zinazoonyeshwa kwa mofimu za kiishio {a} na {e} na dhamira za masharti zikionyeshwa kwa mofimu {ki} na {ngali}.en_US
dc.description.sponsorshipPwani Universityen_US
dc.language.isootheren_US
dc.publisherPwani Universityen_US
dc.subjectNJEOen_US
dc.subjectHALI NA DHAMIRAen_US
dc.subjectKITENZI CHA KITIKUUen_US
dc.titleNJEO, HALI NA DHAMIRA KATIKA KITENZI CHA KITIKUU: MTAZAMO WA UMINIMALISTIen_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record