• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • PhD Thesis and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • PhD Thesis and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    UCHANGANUZI WA NOMINO-MKOPO ZA KIGIRYAMA KUTOKA KIINGEREZA

    Thumbnail
    View/Open
    Ngowa, N,J. 2015 Uchanganuzi wa Nomino mkopo za Kigiryama ku.pdf (801.7Kb)
    Date
    2015-06-05
    Author
    NGOWA, NANCY JUMWA
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Utafiti huu umechanganua kimofofonolojia nomino-mkopo za lugha ya Kigiryama zinazotokana na lugha ya Kiingereza na kubainisha kanuni zinazoongoza michakato mahsusi. Madhumuni ya utafiti huu ni kutambulisha nomino-mkopo zinazotoka katika lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama katika shughuli za ukarabati na vifaa vya magari, pikipiki na baisikeli, kudhihirisha michakato ya kimofofonolojia ambayo inapitiwa na nomino-mkopo hizi na kubainisha kanuni za kimofofonolojia zinazodhibiti ukopaji wa nomino kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. Nadharia ambayo iliongoza uchanganuzi huu ni Fonolojia Zalishi Asilia inayoangaziwa na Hooper (1976). Maeneo ya utafiti yaliyoteuliwa ni Bamba, Kaloleni, Kilifi, Malindi na Galana. Sampuli ya magareji yaliyoteuliwa ni yale yanayopatikana karibu na miji ya maeneo mahsusi. Data ya kimsingi ya utafiti ilikuwa nomino-mkopo za lugha ya Kigiryama zinazotokana na lugha ya Kiingereza. Nomino hizi zinazotokana na vifaa na shughuli mbalimbali za ukarabati zinazoendeshwa katika magereji ya magari, pikipiki na baiskeli. Data ilikusanywa kwa kutumia mbinu ya Uchunguzi Ushirikishi ambapo mtafiti alifanya kazi kama ‘spannerboy’ kwa muda wa wiki moja katika kila gereji lililoteuliwa la makanika Wagiryama na kukusanya data ya nomino-mkopo za lugha ya Kigiryama kupitia mazungumzo na mahojiano yao. Mtafiti alikusanya data kwa kunakili nomino-mkopo moja kwa moja kutoka kwa wazungumzi wenyeji wa lugha ya Kigiryama . Ukusanyaji data pia ulihusisha kurekodi sauti za wazungumzaji ili kuweza kunasa matamshi mahsusi ya nomino-mkopo zilizokusanywa. Data ilichanganuliwa kwa kuzingatia hatua mahsusi. Kwanza nomino-mkopo zilipangwa katika makundi na kunukuliwa kifonetiki. Kisha mabadiliko ya sauti katika v nomino-mkopo hizi yalitambuliwa na sauti mahsusi zinazobadilika kuweza kuthibitishwa. Baadaye ruwaza za mabadiliko ya fonimu zilitambuliwa na hatimaye kanuni zinazotawala michakato mahsusi ya kimofofonolojia ziliweza kuwekwa bayana. Maelezo, ufafanuzi, michoro na majedwali yalitumiwa katika utafiti huu. Tasnifu hii imepagwa katika sura tano. Sura ya kwanza inashughulikia utangulizi wa utafiti kwa kuzingatia misingi ya utafiti huu na kuweka bayana swala la utafiti, madhumuni ya utafiti, nadharia tete, upeo wa utafiti na natija ya utafiti. Katika sura ya pili, misingi ya nadharia ya utafiti huu pamoja na misingi ya kidhana imewekwa bayana. Sura ya tatu inaeleza utaratibu wa utafiti, eneo la utafiti, jumuia na uteuzi wa sampuli, vifaa vya kukusanyia data, utaratibu wa kukusanya data, jinsi data ilivyochanganuliwa, pamoja na kuonyesha uaminiki na maadili yaliyozingatiwa katika utafiti huu. Sura ya nne inashughulikia uchanganuzi wa data na matokeo ya utafiti na sura ya tano inatamatisha utafiti huu kwa kutoa hitimisho la utafiti huu na mapendekezo ya mada zingine zinazoweza kufanyiwa utafiti. Utafiti huu ni mchango muhim katika taaluma ya isimu linganishi kwa jinsi ambavyo unahusisha lugha mbili – Kiingereza na Kigiryama. Zaidi ya hayo, utafiti huu unasaidia katika ufundishaji wa lugha ya pili kwa sababu vikwazo vya kifonolojia vya lugha hizi mbili vimewekwa bayana. Kwa jumla utafiti huu unachangia katika kuweka hai na kuendeleza lugha ya Kigiryama kwa sababu imeweza kupata ukwasi wa istilahi za kuweza kutumika katika uwanja wa kiteknolojia wa ukarabati wa magari, pikipiki na baiskeli. Kwa jumla utafiti huu ni mchango mpya katika tafiti za kiisimu za lugha ya Kigiryama na pia ni hazina kubwa katika uwanja wa Isimu za lugha za Kiafrika.
    URI
    http://elibrary.pu.ac.ke/handle/123456789/740
    Collections
    • Department of Linguistics, Languages and Literature

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV
     

     

    Browse

    All of PUSpaceCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV