• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    ATHARI ZA USASA KWENYE USIMULIZI WA HADITHI KATIKA JAMII YA WAMASAABA NCHINI UGANDA

    Thumbnail
    View/Open
    Wanyenya Willy.pdf (1.507Mb)
    Date
    2018-07-16
    Author
    Willy, Wanyenya
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Kazi hii inahusu athari za usasa katika usimulizi wa hadithi miongoni mwa Wamasaaba nchini Uganda. Swala la utafiti ni kuwa mchango wa usasa katika usimulizi wa hadithi umezua maoni mbalimbali kutoka kwa wasomi tofautitofauti yanayokinzana. Baadhi ya wasomi hao wanaona kuwa usasa umechangia pakubwa sana uimarikaji wa hadithi katika jamii na wengine wanaona kuwa usasa ndio umechangia ufifiaji wa hadithi katika jamii mbalimbali. Kwa hiyo, utafiti huu ulidhamiria kuziba pengo ambalo linasababishwa na maelezo kinzani ya wasomi tofautitofauti kuhusu mchango wa usasa katika usimulizi wa hadithi. Madhumuni katika utafiti huu yalikuwa: Kubainisha mambo ya kisasa ambayo yameshuhudiwa katika jamii mbalimbali kuanzia karne ya 20, kueleza athari za mambo hayo katika usimulizi wa hadithi na kueleza mustakabali wa utamaduni wa kusimulia hadithi katika jamii ya Wamasaaba. Katika kazi hii, mtafiti aliongozwa na nadharia ya usasashaji. Nadharia hii iliasisiwa na Marx (1864). Kwa mujibu wa Marx (1864), nadharia hii hutumiwa kueleza mchakato wa mabadiliko katika jamii kutokana na usasa. Mkabala wa utafiti katika kazi hii ulikuwa wa nyanjani. Mtafiti alitumia mkabala huu kwa sababu ulikuwa njia ya pekee ambayo ingemleta pamoja na wazee wenye maarifa ambayo wangempa maneno ya busara. Kwa kutumia mkabala huu, mtafiti alizuru nyanjani halafu akaendeleza mahojiano na wahojiwa pamoja na kusambaza hojaji. Mahojiano yaliyoendelezwa yalimwezesha mtafiti kukusanya taarifa mbalimbali kuhusu hadithi miongoni mwa Wamasaaba. Taarifa zilizokusanywa zilijumulisha maelezo kuhusu mambo ya kisasa ambayo yameshuhudiwa katika jamii ya Wamasaaba kuanzia karne ya 20 hadi sasa, athari zake katika usimulizi wa hadithi na mustakabali wa utamaduni wa kusimulia hadithi katika jamii hiyo. Kwa jumla
    URI
    http://elibrary.pu.ac.ke/handle/123456789/776
    Collections
    • Department of Linguistics, Languages and Literature

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV
     

     

    Browse

    All of PUSpaceCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV