• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    MITAZAMO YA WAANDISHI WA KIKE NA WA KIUME KUHUSU USAWIRI WA WAHUSIKA WA KIKE KATIKA TAMTHILIA ZA KISWAHILI

    Thumbnail
    View/Open
    JOHN MUTUA FINAL.pdf (1.862Mb)
    Date
    2017-10-12
    Author
    MUTUA, JOHN MUSYOKA
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa ni kuchunguza mitazamo ya waandishi wa kike na wa kiume kuhusu usawiri wa wahusika wa kike katika tamthilia za Kiswahili. Mtafiti aliongozwa na malengo matatu. Kwanza, ni kutambulisha jinsi waandishi wa kike walivyowasawiri wahusika wa kike katika tamthilia zilizoteuliwa. Pili, kuonyesha jinsi waandishi wa kiume walivyowasawiri wahusika wa kike katika tamthilia zilizoteuliwa.Mwisho, ni kulinganisha na kubainisha mitazamo ya waandishi hao kama walivyowasawiri wahusika wa kike. Sifa mbalimbali waandishi hao walizowapa wahusika wa kike katika tamthilia zao, zimeonyesha tofauti za kimitazamo baina yao. Aidha, utafiti huu umeonyesha waandishi walio na mitazamo chanya na vilevile walio na mitazamo hasi kwa wahusika wa kike. Matokeo ya utafiti huu yameonyesha kuwa waandishi wa kike huwasawiri wahusika wa kike kwa mtazamo hasi katika tamthilia za Kiswahili. Pia, umeonyesha baaadhi ya sababu ambazo yamkini ndizo zilizowachochea baadhi ya waandishi kuwa na mitazamo tofauti kuhusu wahusika wa kike kwenye kazi zao za kifasihi. Utafiti uliongozwa na nadharia ya Ufeministi wa Baada-ukoloni inayohusishwa Said (1993) na baadaye kutiwa nguvu na Mills (1995). Nadharia hii inasaili jinsi mataifa ya kimagharibi yalivyousawiri utamaduni wa nchi za Kiafrika. Nadharia hii inadai kuwa mtagusano wa kitamaduni baina ya mataifa tawala na mataifa tawaliwa ulisababisha athari kuhusu mahusiano ya kijinsia barani Afrika. Kwa hivyo, usawiri wa wahusika wa kike katika mataifa ya ulimwengu wa tatu ni mwigo wa mitazamo ya wakoloni waliotawala barani Afrika kabla ya uhuru. Tasnifu hii imegawanywa katika sura tano. Sura ya kwanza imeshughulikia usuli wa mada, madhumuni ya utafiti, maswali ya utafiti, upeo, natija ya utafiti na maelezo ya vi istilahi. Sura ya pili inajumuisha mapitio ya maandiko na msingi wa nadharia. Sura ya tatu, inahusu mbinu za utafiti na ukusanyaji wa data, utaratibu wa utafiti, jumuiya na uteuzi wa sampuli. Aidha, inahusu mbinu za ukusanyaji data, vifaa vya kukusanyia data, uchanganuzi wa data, maadili ya utafiti, uaminikaji na utegemewaji wa utafiti na msingi wa kidhana. Sura ya nne imegawanyika katika sehemu tatu. Kwanza, ni mitazamo ya waandishi wa kike. Pili, ni mitazamo ya waandishi wa kiume na tatu, ulinganishaji wa mitazamo ya waandishi kijinsia. Sura ya tano ni hitimisho, sababu za usawiri na mapendekezo. Utafiti huu umefanywa maktabani. Mbinu zilizotumiwa ni; upekuzi wa makala na matini mbalimbali, usomaji wa tamthilia zilizohusika, kunakili na kuorodhesha sifa za wahusika wa kike. Aidha, michoro, chati, majedwali na tarakimu zilitumiwa kuwakilisha hali mbalimbali. Utafiti huu utawanufaisha wasomaji na wahakiki wa kazi za kifasihi. Kwanza, umebainisha mitazamo tofauti ya waandishi wa tamthilia za Kiswahili. Umeonyesha kuwa waandishi wa kike wanawasawiri wahusika wa kike kwa mtazamo hasi zaidi wakilinganishwa na waandishi wa kiume. Halikadhalika, umekuwa tathmini ya juhudi za waandishi wa tamthilia za Kiswahili katika kuibadilisha taswira ya mwanamke katika fasihi na jamii. Pia, ni mchango katika mdahalo wa mahusiano ya kinjisia unaoendelea kote ulimwenguni. Mtafiti amehakiki tamthilia nne. Mbili za waandishi wa kike ambao ni Katini Mwachofi; Mama Ee na Catherine Kisovi aliyeandika Dunia Hadaa. Waandishi wa kiume ni Alamin Mazrui na Kimani Njogu ambao wameandika
    URI
    http://elibrary.pu.ac.ke/handle/123456789/793
    Collections
    • Department of Linguistics, Languages and Literature

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV
     

     

    Browse

    All of PUSpaceCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV