• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    UCHANGANUZI WA ATHARI ZA KIMOFOFONOLOJIA MIONGONI MWA WANAFUNZI WA KISOMALI WANAPOJIFUNZA LUGHA YA KISWAHILI

    Thumbnail
    View/Open
    Amos Kativa Manundu.pdf (949.4Kb)
    Date
    2019-07-28
    Author
    MANUNDU, AMOS KATIVA
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Utafiti huu ulishughulikia makosa ya kimofofonolojia miongoni mwa wanafunzi wa Kisomali wanapojifunza Kiswahili sanifu kama lugha yao ya pili. Utafiti huu ulifanywa katika shule za upili za umma katika kaunti–ndogo ya Garissa-Township, Garissa kaunti, nchini Kenya. Lugha ya Kisomali imefanyiwa utafiti katika vipengele mbalimbali katika maeneo tofautitofauti lakini hakuna utafiti ambao umewahi kufanywa katika maeneo ya Garissa. Basi utafiti huu ulilenga kuziba mwanya huu wa kielimu hasa katika kiwango cha kimofofonolojia katika lugha ya Kisomali, eneo la Garissa. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) ambayo iliasisiwa na Corder mwaka wa 1967, ambaye anasema kuwa kufanya kosa ni njia mojawapo ya kujifundisha lugha ya pili. Kwa hivyo, mwanafunzi anapofanya kosa, asiadhibiwe bali chanzo cha kosa kibainishwe. Data iliyohusishwa ilitoka nyanjani na ilikuwa makosa ya kimofofonolojia katika lugha ya Kiswahili yanayofanywa na wanafunzi wenye asili ya lugha ya Kisomali kutoka shule za upili za umma za kaunti-ndogo ya Garissa-Township. Data ya nyanjani ilikusanywa kwa kutumia mbinu ya kuandika insha na kusimulia hadithi ambapo wanafunzi wa kidato cha tatu waliokuwa wameteuliwa waliandika insha na kusimulia hadithi. Wanafunzi hawa waliteuliwa kwa sababu walikisiwa kuwa wamepata umilisi wa lugha ya Kiswahili na hawakuwa katika pilka pilka za kujiandaa kwa mtihani wa kitaifa. Mtafiti alikusanya insha ili kuzisoma na kanda alizokuwa amerekodi ili kuzisikiliza na kutambua makosa ya kimofofonolojia yaliyofanywa na wanafunzi. Hii ndio ilikuwa data ya utafiti. Data ilichanganuliwa kwa kutumia uchanganuzi wa maelezo. Vifaa tulivyotumiwa ni insha na hadithi.
    URI
    http://elibrary.pu.ac.ke/handle/123456789/823
    Collections
    • Department of Linguistics, Languages and Literature

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV
     

     

    Browse

    All of PUSpaceCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV