• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    •   Repository Home
    • Electronic Theses and Dissertations
    • Masters Theses and Dissertations
    • Department of Linguistics, Languages and Literature
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    MNYAMBULIKO WA VITENZI KATIKA LUGHA YA KIDIGO: MKABALA WA FONOLOJIA ZALISHI ASILIA

    Thumbnail
    View/Open
    MWAMZANDI SUMAIYA YUNUS.pdf (1.018Mb)
    Date
    2022-04-21
    Author
    MWAMZANDI, SUMAIYA YUNUS
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Utafiti huu ulihusu mnyambuliko wa vitenzi katika lugha ya Kidigo kwa madhumuni ya kubainisha kanuni zinaohusika katika mchakato wa kunyambua vitenzi katika lugha hii. Kama lugha mojawapo ya Kibantu, lugha ya Kidigo ni miongoni mwa lugha ambayo haijatafitiwa kwa upana hasa katika maswala ya kiisimu. Mnyambuliko wa vitenzi umefanywa katika lugha mbalimbali za Kibantu ikiwemo Kigiriama, Kikuria, Kirunyankole na kadhalika lakini haujafanywa katika lugha ya Kidigo. Utafiti huu hivyo unanuia kuziba pengo hili. Malengo ya utafiti huu ni kubainisha mofimu za unyambuaji katika vitenzi vya Kidigo kwa kutumia kauli mbalimbali, kuchambua mifanyiko ya kimofofonolojia katika vitenzi vilivyonyambuliwa na kueleza kanuni za kimofofonolojia zinazodhibiti mnyambuliko wa vitenzi vyenye asili ya lugha ya Kidigo. Umuhimu wa utafiti huu ni kupambanua lugha ya Kidigo kwa misingi ya kiisimu ili kuweka misingi thabiti ya sarufi ya lugha hii na vilevile kuongeza idadi ya tafiti zilizofanywa katika lugha ya Kidigo. Data ya utafiti huu ni vitenzi vyenye asili ya Kidigo na vilikusanywa kutoka nyanjani. Vitenzi vilikusanywa eneo la Msambweni katika kaunti ya Kwale kwa njia ya mahojiano ambapo mtafiti alishiriki katika kuuliza maswali ili apate data yake. Data hii baadae ilipangwa na kuchanganuliwa kwa misingi ya Nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia ili kubainisha sheria zilizohusika na mnyambuliko wa vitenzi katika lugha ya Kidigo. Mifanyiko ya kimofofonolojia iliyodhihirika baada ya kunyambua vitenzi vya Kidigo ni sita nayo ni: uwiano wa irabu, uchopekaji, udondoshaji, ubadala wa fonimu, kuimarika na kudhoofika kwa fonimu. Uchanganizi huu ulifanywa kwa njia ya maelezo yakisaidiwa na michoro pamoja na majedwali. Matokea ya utafiti yalionyesha kuwa lugha ya Kidigo ni lugha nyambulishi kwa jinsi ambavyo vitenzi viliweza kunyambulika katika kauli mbalimbali. Utafiti pia uliweza kudhihirisha kuwa shughuli ya mnyambuliko wa vitenzi katika lugha ya Kidigo huhusisha mifanyiko mbalimbali ya kimofofonolojia inayoongozwa na sheria maalum
    URI
    http://elibrary.pu.ac.ke/handle/123456789/988
    Collections
    • Department of Linguistics, Languages and Literature

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV
     

     

    Browse

    All of PUSpaceCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    DSpace software copyright © 2002-2016  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    Atmire NV